Tuesday, 25 October 2016

TAFAKARI Jumatano ya 30 ya Mwaka - C "Mlango wa kuingia katika ufalme wa Mungu".


TAFAKARI
      Jumatano, Oktoba 26, 2016,
     Juma la 30 la Mwaka wa Kanisa
 
        Efe 6:1-9;
            Zab 144:10-14;
              Lk 13:22-30
 
     
           MLANGO WAKUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU!

             Mungu ametuandalia maisha ya uzima wa milele na maisha haya ni kwa ajili ya wote. Yesu anasema katika Injili ya leo, “Nao watakuja watu toka mashariki na magharibi, na toka kaskazini na kusini, nao wataketi chakulani katika ufalme wa Mungu” (Lk 13:29).
Kitu kimoja ambacho ni hakika ni kwamba hakuna upendeleo katika Ufalme wa Mungu. Petro anatuambia katika Kitabu cha matendo ya Mitume, “kwa hakika ninajua Mungu hana upendeleo, bali katika kila taifa anayemuogopa yeye nakufanya yalio haki anakubaliwa naye. (Mdo10:34-35).
Hivyo yule mtu alivyo muuliza Yesu, “je ni wachache watakao okolewa ?”. Yesu hakumjibu moja kwa moja. Yesu hasemi ni wachache au wengi, hawa au wale, anasema tu “jitahidini kuingia katika mlango mwembamba” . (Lk 13:23-24). Kwahiyo kwa kadiri ya Yesu ni kwa wale wanaojitahidi kuingia kupitia mlango huo watakao ingia. Na kwasababu mlango wa kuingia katika uzima wa milele ni mwembamba, waweza kujichunguza ni mizigo mingapi uliobeba ambayo yaweza kukuzuia kuingia, usije kukumbwa na mshangao. Yesu anasema “Na tazama, wako walio wa mwisho watakaokuwa wa kwanza, na wa kwanza watakaokuwa wa mwisho” (Lk 13:30). Walioteuliwa waweza kuwa wa mwisho.
Watu kutoka kaskazini na kusini, magharibi na Mashariki waweza kuwatangulia. Kwahiyo, wale wanaodhani wana nafasi ya pekee katika Ufalme wa Mungu kwasababu tuu wana elimu kuhusu Yesu, au kwasababu wanaenda kanisani kila jumapili, au kwasababu wamesikia mahubiri ya kila jumapili wasije wakashangaa ikawa kinyume. Hili ndilo onyo la Yesu. Kwa njia nyingine tuangalie sana kama kila tunalotenda ni kwa ajili ya ufalme wa Mungu na kumrudishia yeye utukufu au ni kwa ajili ya utukufu binafsi? Manake twaweza kufanya yote vyema ili tuonekane machoni pa watu na kusifiwa na wanadamu, tukajijengea utukufu binafsi! Kwa njia hii tusishangae siku ya mwisho.

       Sala: Bwana Yesu, asante kwa zawadi ya ukombozi. Naomba unipe neema ili niweze kuwa miongoni mwao wote watakao okolewa nawe nakuingia katika Ufalme wako. Amina.

Copyright © 2016 Shajara and published by MAMBO YAHUSUYO IMANI BLOG
      see: imani-katoliki.blogspot.com

1 comment:

  1. Hakika, hali ya kiroho hudhibiti mambo ya kimwili.

    Mimi na mume wangu tulikuwa tumeoana kwa zaidi ya miaka 8 bila kupata mtoto. Tulitembelea hospitali tofauti, lakini kimatibabu sote tulikuwa sawa, lakini mimba haikutokea. Siku moja, nilikutana na mpenzi wangu wa zamani. Tulitumia muda pamoja, tukazungumza kuhusu yaliyopita, na hatimaye tukafanya ngono. Baadaye, nikapata mimba. Nilichanganyikiwa na sikujua la kufanya.

    Nilijua mtoto hakuwa wa mume wangu, lakini kwa udadisi, nilifanya kipimo cha ubaba kwa siri bila idhini ya mume wangu, na matokeo yakathibitisha kwamba hakuwa baba mzazi. Hata hivyo, sikutaka kuharibu ndoa yangu au kuharibu furaha na furaha ambayo mtoto alileta kwa familia yetu, hasa mama mkwe wangu.

    Rafiki yangu kisha akanipendekeza mtaalamu wa mizimu mwenye nguvu. Niliwasiliana naye na kumuelezea kila kitu, Alinipa maagizo, ambayo nilifuata, na akafanya ibada ambayo ilitakiwa kufanya kipimo cha ubaba kilingane na mume wangu na kufanya damu ilingane na yake. Mwanzoni, sikuamini kwa sababu ilisikika kuwa ya ajabu.
    Miezi sita baada ya ibada, tulifanya mtihani mwingine wa ubaba, na kwa mshangao wangu, matokeo yalionyesha kuwa mtoto sasa alikuwa wa mume wangu.

    Nataka kutumia fursa hii kumthamini mtaalamu wa mizimu.

    Ninampendekeza. Ikiwa unahitaji ibada ili kupata mimba haraka.

    .Ibada ya kumrudisha mwenzi wako wa zamani.

    Ibada ya kurejesha urithi wako/kushinda bahati nasibu na zaidi.

    Maelezo yake. wightmagicmaster@gmail.com

    WhatsApp: +2349046229159

    ReplyDelete

"Asante sana kwa maoni yako"

NYIMBO ZA DOMINIKA YA 29 YA MWAKA- C WA KANISA.

Nyimbo za Jumapili ya 29 Mwaka C Karibu kwa ajili ya nyimbo za Jumapili ya 29 Mwaka "C" Mwanzo: Ee Bwana Nimekuita  ...