Tuesday, 25 October 2016
MASOMO YA MISA, 25/10/2016 Jumanne ya 30 ya Mwaka - C
MASOMO YA MISA,
OKTOBA 25, 2016 JUMANNE,
JUMA LA 30 LA MWAKA WA KANISA
SOMO 1
Efe. 5:21 – 33
Hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo. Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo, vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo. Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; apate kujiletea Kanisa atukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wal alolote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa. Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda wenyewe. Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake popote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye navyolitendea Kanisa. Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa. Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 128:1 – 5 (K)
(K) Heri kila mtu amchaye Bwana.
Heri kila mtu amchaye Bwana, Aendaye katika njia yake. Taabu ya mikono yako hakika utaila; Utakuwa heri, na kwako kwema. (K)
Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao, Vyumbani mwa nyumba yako. Wanao kama miche ya mizeituni Wakiizunguka meza yako. (K)
Tazama, atabarikiwa hivyo, yule amchaye Bwana. Bwana akubariki toka Sayuni; Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako. (K)
SHANGILIO
1Pet. 1:25
Aleluya, aleluya, Neno la Bwana hudumu hata milele, na neno hilo ni neno lile jema lililohubiriwa kwenu. Aleluya.
INJILI
Lk. 13:18-21
Yesu alisema, Ufalme wa Mungu umefanana na nini? Nami niufananishe na nini? Umefanana na punji ya haradali aliyotwaa mtu akaitupa katika shamba lake; ikamea, ikawa mti; ndege wa angani wakakaa katika matawi yake. Akasema mara ya pili, Niufananishe na nini ufalme wa Mungu? Umefanana na chachu aliyotwaa mwanamke akaisitiri ndani ya pichi tatu za unga, hata ukachacha wote pia.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
NYIMBO ZA DOMINIKA YA 29 YA MWAKA- C WA KANISA.
Nyimbo za Jumapili ya 29 Mwaka C Karibu kwa ajili ya nyimbo za Jumapili ya 29 Mwaka "C" Mwanzo: Ee Bwana Nimekuita ...
-
Katika kuhakikisha kwamba uinjili shaji unakua tumekuletea nata zanyimbo za kikatoliki hizihapa Bofya hapa ...
-
Nyimbo za Jumapili ya 29 Mwaka C Karibu kwa ajili ya nyimbo za Jumapili ya 29 Mwaka "C" Mwanzo: Ee Bwana Nimekuita ...
-
Dominika ya 28 ya Mwaka SOMO LA 1 2 Fal 5:14-17 Naamani alishuka, akajichovya mara saba katika Y...
-
Dominika ya 30 ya Mwaka SOMO LA 1 Ybs 35:12-14,16-19 Kwa kuwa Bwana ndiye mhukumu wala hakijali cheo cha mtu. Hatamkubali ye yote juu...
-
Dominika 29 ya Mwaka SOMO LA 1 Kut 17:8-13 Wakati huo Waamaleki wakatokea, wakapigana na Israeli huko Ref...

Hakika, hali ya kiroho hudhibiti mambo ya kimwili.
ReplyDeleteMimi na mume wangu tulikuwa tumeoana kwa zaidi ya miaka 8 bila kupata mtoto. Tulitembelea hospitali tofauti, lakini kimatibabu sote tulikuwa sawa, lakini mimba haikutokea. Siku moja, nilikutana na mpenzi wangu wa zamani. Tulitumia muda pamoja, tukazungumza kuhusu yaliyopita, na hatimaye tukafanya ngono. Baadaye, nikapata mimba. Nilichanganyikiwa na sikujua la kufanya.
Nilijua mtoto hakuwa wa mume wangu, lakini kwa udadisi, nilifanya kipimo cha ubaba kwa siri bila idhini ya mume wangu, na matokeo yakathibitisha kwamba hakuwa baba mzazi. Hata hivyo, sikutaka kuharibu ndoa yangu au kuharibu furaha na furaha ambayo mtoto alileta kwa familia yetu, hasa mama mkwe wangu.
Rafiki yangu kisha akanipendekeza mtaalamu wa mizimu mwenye nguvu. Niliwasiliana naye na kumuelezea kila kitu, Alinipa maagizo, ambayo nilifuata, na akafanya ibada ambayo ilitakiwa kufanya kipimo cha ubaba kilingane na mume wangu na kufanya damu ilingane na yake. Mwanzoni, sikuamini kwa sababu ilisikika kuwa ya ajabu.
Miezi sita baada ya ibada, tulifanya mtihani mwingine wa ubaba, na kwa mshangao wangu, matokeo yalionyesha kuwa mtoto sasa alikuwa wa mume wangu.
Nataka kutumia fursa hii kumthamini mtaalamu wa mizimu.
Ninampendekeza. Ikiwa unahitaji ibada ili kupata mimba haraka.
.Ibada ya kumrudisha mwenzi wako wa zamani.
Ibada ya kurejesha urithi wako/kushinda bahati nasibu na zaidi.
Maelezo yake. wightmagicmaster@gmail.com
WhatsApp: +2349046229159