Saturday, 24 September 2016

TAFAKARI: 24/9/2016 Juma la 25 la Mwaka. " Ubatili mtupu; mambo yote ni ubatili, Mhubiri asema!” (Muh 12: 8)."


Jumamosi, Septemba 24, 2016.
Juma la 25 la Mwaka

      Mhu 11: 9 - 12: 8
   Zab 89: 3-6, 14, 17
      Lk 9: 43-45

     UBATILI: MAISHA BILA MUNGU! “Ubatili mtupu; mambo yote ni ubatili, Mhubiri asema!” (Muh 12: 8).

         Kitu ambacho Mwandishi anakiita ubatili ni maisha bila hofu ya Mungu. Maisha ya kufurahia maisha na zawadi zote tulizo pewa bila kujali nafasi ya mwenzangu (jirani) ambapo mtu anakuwa kipofu kuhusu mahitaji ya wengine. Lakini maisha anayoishi mtu kwa ajili ya Mungu na kwa ajili ya watu wake, yanakubalika sana na yana matunda mengi. Yesu leo katika somo la Injili anaongelea kuhusu kifo chake. Lakini mitume hawakuelewa fumbo hili kuu. Yesu alimpenda Baba yake sana kiasi kwamba alikuwa akijiandaa kutimiza mapenzi yake. Nasi ndicho tunachopaswa kufanya, tunapaswa tujitahidi kuyajua mapenzi ya Mungu kwetu na kujaribu kuyatimiza katika maisha yetu. Na hapo maisha yetu hayatakuwa maisha ya ubatili. Sala: Bwana mpendwa, tubariki wote na tuongoze ili tuweze kutambua mapenzi yako kwetu ili tuweze kuongozwa na maisha ya fadhila. Amina

Copyright © by shajara and published by MAMBO YAHUSUYO IMANI BLOG

No comments:

Post a Comment

"Asante sana kwa maoni yako"

NYIMBO ZA DOMINIKA YA 29 YA MWAKA- C WA KANISA.

Nyimbo za Jumapili ya 29 Mwaka C Karibu kwa ajili ya nyimbo za Jumapili ya 29 Mwaka "C" Mwanzo: Ee Bwana Nimekuita  ...