Wednesday, 21 September 2016
TAFAKARI YA MASOMO YA MISA,21/9/2016. Jumatano ya 25 ya Mwaka.
Jumatano, Septemba 21, 2016.
Juma la 25 la Mwaka
Sikukuu ya Mt. Mathayo, Mtume na Mwinjili
Efe 4:1-7, 11-13
Zab 19:1-4
Mt 9: 9-13
MUNGU HAWAITI WAKAMILIFU, ANAWAPA UKAMILIFU WALE ALIO WAITA
Leo tuna sheherekea sikukuu ya Mtakatifu Matayo, mmoja wapo wa mitume kumi na mbili wa Bwana wetu Yesu Kristo. Alikuwa mtoza ushuru, alijulikana kama Lawi. Hapa anaitwa Matayo, maana yake “zawadi ya Mungu au aliyetolewa na Mungu”. Kama wale wakwanza wanne walio itwa na Yesu kwanza, Matayo, mtoza ushuru, aliacha kila kitu alichokuwa nacho na akamfuata Yesu. Wakati wa Yesu watu maarufu na watoza ushuru walikataliwa kama wadhambi kwa Wayahudi kadhalika na kwa Wayunani. Walikuwa na picha mbaya kiasa kwamba hata waombaji (omba omba) wenyewe walikataa kuomba chochote kutoka kwao. Ni katika utamaduni huu, Yesu alimuita Matayo/Lawi. Hii ni hali mpya ya kimapinduzi anayo fanya Yesu ili kujenga familia mpya ya Mungu.
Kuna vitu viwili tunaweza kujifunza kutoka kwa Matayo. Cha kwanza, alikubali mwenyewe wito wa Yesu. Wakati Mungu anapo ongea mmoja anaweza kupata kishawishi cha kusema ‘kesho; bado sijawa tayari’. Lakini Matayo mara moja aliitika wito wa Yesu. La pili, Matayo anaitwa akiwa katika mazingira ya hali yake ya maisha ya kawaida, wakati akijishughulisha na kazi yake. Yesu pia aliwaita mitume wa kwanza, Petro na Adrea, Yakobo na Yohane wakati wakiwa wakivua samaki. Leo tutambue kwamba sisi ni wadhambi lakini bado Mungu anatupenda, tumuombe nguvu zake na neema zake ili tuwe na maisha yenye kustahili wito wake.
Sala: Bwana Yesu, tusaidie tuweze kuitika wito wako na tutangaze ujumbe wa Amani na upendo. Amina
Copy right © by shajara and published by MAMBO YAHUSUYO IMANI BLOG
website:
imani-katoliki.blogspot.com
MASOMO YA MISA,21/9/2016. Jumatano ya 25 ya Mwaka-C
MASOMO YA MISA
JUMATANO, SEPTEMBA 21, 2016
JUMA LA 25 LA MWAKA
Sikukuu ya Mt. Mathayo, Mtume na Mwinjili
SOMO 1
Efe. 4:1 – 7, 11 – 13
Nawasihi, mimi niliye mfungwa katika Bwana, mwenende kama inavyoustahili wito wenu mlioitiwa; kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo; na kujitahidi kuuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani, mwili mmoja, na Roho mmoja, Imani moja, ubatizo mmoja. Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote. Lakini kila mmoja wenu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa chake Kristo. Naye alitoa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti; na wengine kuwa wachungaji na waalimu; kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa Imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 19:1 – 4 (K) 4
(K) Sauti yao imeenea duniani mwote.
Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu,
Na anga laitangaza kazi ya mikono yake.
Mchana husemezana na mchana,
Usiku hutolea usiku maarifa. (K)
Hakuna lugha wala maneno,
Sauti yao haisikilikani.
Sauti yao imeenea duniani mwote,
Na maneno yao hata miisho ya ulimwengu. (K)
SHANGILIO
Aleluya, aleluya,
Ee Mungu, tunakusifu,
tunakukiri kuwa Bwana.
Jamii tukufu ya Mitume inakusifu.
Aleluya.
INJILI
Mt. 9:9 – 13
Yesu alipokuwa akipita aliona mtu ameketi forodhani, aitwaye Mathayo, akamwambia, Nifuate. Akaondoka, akamfuata. Ikawa alipoketi nyumbani ale chakula, tazama, watoza ushuru wengi na wenye dhambi walikuja wakaketi pamoja na Yesu na wanafunzi wake. Mafarisayo walipoona, waliwaambia wanafunzi wake, Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi? Naye aliposikia, aliwaambia, Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio hawawezi. Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, Nataka rehema, wala si sadaka; kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.
Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
Copy right© by shajara and published by MAMBO YAHUSUYO IMANI BLOG
website:
Subscribe to:
Posts (Atom)
NYIMBO ZA DOMINIKA YA 29 YA MWAKA- C WA KANISA.
Nyimbo za Jumapili ya 29 Mwaka C Karibu kwa ajili ya nyimbo za Jumapili ya 29 Mwaka "C" Mwanzo: Ee Bwana Nimekuita ...
-
Katika kuhakikisha kwamba uinjili shaji unakua tumekuletea nata zanyimbo za kikatoliki hizihapa Bofya hapa ...
-
JUMAPILI YA 28 YA MWAKA-C Somo I: 2Fal 5:14-17 Zab/Kit: 98:1-2, 3ab, 3cd-4 Somo II: 2Tim 2:8-13 Injili: Lk 17:11-19 Nukuu ...
-
Nyimbo za Jumapili ya 29 Mwaka C Karibu kwa ajili ya nyimbo za Jumapili ya 29 Mwaka "C" Mwanzo: Ee Bwana Nimekuita ...
-
Dominika ya 28 ya Mwaka SOMO LA 1 2 Fal 5:14-17 Naamani alishuka, akajichovya mara saba katika Y...
-
Dominika ya 30 ya Mwaka SOMO LA 1 Ybs 35:12-14,16-19 Kwa kuwa Bwana ndiye mhukumu wala hakijali cheo cha mtu. Hatamkubali ye yote juu...

